MJI wa Songea jana ulizizima kwa mapokezi makubwa ya
viongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo wakiongozwa na kiongozi wa chama hicho Zitto Kabwe. Zitto, ambaye ameambatana na viongozi wengine wa juu wa ACT akiwemo Mwenyekiti wa ACT Taifa, Anna Mghwira pamoja na Katibu Mkuu wake Samson Mwigamba. Viongosi hao walisili jana mjini hapa ambapo walilakiwa na mamia ya wananchi wa mji wa Songea wakiongozwa na vijana wa bodaboda zaidi ya 300. Akihutubia mamia ya wananchi jana mjini Songea katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya Malori Majengo, Zitto, alisema lengo la kuanza ziara mkoani Ruvuma ikiwa kuenzi na kutekelza kwa vitendo azimo la Songea. Alisema na hilo pia mkoa huo una historia ya ukombozi wa vita ya majimaji iliyoanzia wilayani Kilwa na baadaye kuenea hadi Songea. Mbunge huyo wa zamani ya Kigoma Kaskazini, alisema kutokana na hali hiyo ACT-Wazalendo wameanza ziara hiyo ili kupata baraka za mababu wa ukombozi na si kushindana au kuviponda vyama vingine vya siasa. Alisema kitendo cha baadhi ya watu kufikiri kuwa ziara yake ina lengo la mashambulizi si sahihi bali sasa ni changamoto kwa wakazi wa mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanapanda viongozi wa upinzani kama njia ya kustawisha demokrasia nchini. Ruvuma ni Mkoa ambao hauna mbunge wa upinzani hata mmoja na tumeona tutume salamu kwa umma huku lengo letu likiwa
likiwa kuingoa CCM madarakani na kwamba hatuna nia ya
kugambana na vyama vingine. Wakazi wa Songea ni wajibu wenu kupima je pamoja na historia ya ukombozi ambayo ACT-Wazalenzo tunaamini ndio misingi ya ukombozi wan chi yetu je kukosa mbunge hata mmoja wa upinzani ni sahihi, hili ni lazima tulikate na tufanye uamuzi huo sasa hasa kuelekea Oktoba mwaka huu, alisema Zitto. Akizungumzia Mkoa wa Ruvuma kama mmoja wa mikoa mitano inayotegemewa kwa uzalishaji mkubwa wa chakula, alisema pamoja na wakulima kuhangaika usiku na mchana lakini bado hakuna juhusu za Serikali za kuwakomboa katika lindi la umaskini ili wafurahie kilimo chao. Alisema kwa muda sasa bei za mazao zimekuwa zikishuka lakini bado Serikali imeshindwa kuwalipa wakulima Sh bilioni 13 za mahindi bila kuwa na utaratibu madhubuti wa kulipa madeni hayo. Kwan chi zilizoendelea zimekuwa zikithamini juhudi zinazofanywa na wakulima ikiwemo kuundiwa mfuko wa mazao, ambao unafanya kazi ya kuhakikisha dhamani ya mazao inalindwa. Ikitoa bei ya mazao inashuka linakua jukumu la mfuko kulipa fidia ya hasara kwa wakulima, ambapo hili huenda sambamba na kuwepo kwa mfuko huo ambao. Nasi ACT- Wazalendo tungependa kuonyesha sera yetu ya hifadhi ya jamii ambapo kila mkulima awe na bima ya afya. Mpango wetu ni kwamba kama mchango wa hifadhi ya jamii ni Sh 30,000 basi Serikali itamchangia mkulima Sh 10,000, alisema Zitto .
Alisema kutokana na changamoto za wakulima wanataka
kuonyesha wana majawabu ambapo mkulima atatibiwa bure akiwa na hifadhi ya jamii na uhakika wa bei kupitia mfumuko wa bei katika hifadhi ya jamii. Utafiti wa Shirikala la Kazi Duniani (ILO), wa mwaka 2013 unaonyesha kuwa nchi ambazo zimesambaza hiafdhi ya jamii kwa wananchi wake wote zimeondoka kwenye umaskini kwa kasi na ukiaji wa uchumi unaongezeka mara dufu, alisema Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo.