Escolar Documentos
Profissional Documentos
Cultura Documentos
ISSN 0856 - 3861 Na. 1045 MUHARRAM 1434, IJUMAA NOVEMBA 16-22, 2012 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Mhariri wa gazeti la ANNUUR wa watendaji wake wanawatakia kheri ya Mwaka Mpya wa Kiislamu 1434 Hijiria
Lipumba ahoa nchi Mamlaka ya Zanzibar lazima kutekwa na masadi Kiti chake Umoja wa Mataifa bado kipo Adai wanakimbilia pato la gesi
DAUDI Kapaya (wa pili kutoka kushoto) akiwa mahakamani Kisutu jana.
jana alikishwa katika mahakama ya Kisutu D A U D I K a p a y a , kwa ajili ya kesi ya mwenye umri wa miaka k u k o j o l e a Q u r a n 20 mkazi wa Ukonga inayomkabili. Majumba Sita, kitongoji Hata hivyo katika hali ya cha Mogo Mkengeni, Inaendelea Uk. 4
2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0755 260 087 0713 110148, DSM. www.ipctz.org E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
Tahariri/Habari
AN-NUUR
AN-NUUR
MAONI YETU
MAKAMO wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maaalim Seif Sharif Hamad. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa hilo ushirikiano wa kimataifa halimo katika article of union wamelipenyeza, alisema na kuendelea: Kwa hivyo wametukata miguu na unapeleka nyaraka za kusaidiwa zinaganda kwao, kwa hivyo Muungano huu hautufai Wazanzibari, hao wenye kusema Serikali hizi lazima tunawaambia lazima ni Mwenyezi Mungu tu, hilo unalisema wewe tu, nani kakutuma ukaseme hivyo, alisema maalim Seif. Maalim Seif, alisema Waziri Mkuu wa Tanzania mheshimiwa Mizengo Pinda, amekuwa akitoa vitisho dhidi ya watu wanaohitaji mabadiliko ya Muungano ili Zanzibar iwe na mamlaka yake kamili: Mheshimiwa Pinda, anatoa vitisho anasema Muungano wetu umeshakomaa kukomaa kwa maana ya kupea sio kama ukomasasa anasema laa Mtanganyika awe Mtanganyika, Wazanzibari warudi kwaokakwambia nani Pindaaaa, au ndiyo vitisho?, alihoji Maalim Seif. Alisema kwa sasa Mzanzibari hatishiki tena, wakati wa vitisho umekwisha: Mimi nawambia wananchi sababu za Muungano huu ni kuunganisha nchi za Afrika, hebu nambieni nani amekuja kujiunga?, aliuliza na kuendelea: Kuna wakati baadhi ya viongozi wa Afrika walitaka kujiunga, wala haji. Maana kuna wakati Mzee Kaunda, alikuja akachungulia, lakini akasema aaaa sitaki, alisema Maalim Seif. Kuhusu wafanyakzi katika Balozi za Tanzania nchi za nje, alisema hakuna uwiano wa kuridhisha baina ya wafanyakazi katika osi hizo na wote wanatoka upande mmoja wa Muungano: Nilikuwa huko Ulaya kuna maosa 23 Mzanzibari mmoja tu na Umoja wa Mataifa ndiyo kwanza kapelekwa juzi Muombwa, ukenda Uingereza kati ya 19 wote Mzanzibari mmoja, jee hiyo ni haki? Aliuliza na kuendela: Lakini watu wameshika Serikali mbili, yagujuuu!! tunasema tunadai na kudai haki sio vibaya na niwaambie kuna nchi ya Misri na Syria na Syria walipoona mambo hayendi vizuri wakajitoa wala hawakujitoa juzi nilishangaa mheshimiwa Pinda anatoa vitisho, alisema Maalim Seif.
Habari
AN-NUUR
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, amesema kuwa mtandao wa kifisadi unajiandaa kuiteka CCM, baada ya kujua kwamba kuna mali ya asili ya kutosha nchini hasa baada ya kugunduliwa gesi nyingi nchini, hivyo unajipanga mapema kuchukua madaraka ili kuisidi nchi. Prof. Lipumba alisema hayo wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Bagamoyo hivi karibuni. Mtandao umejipanga watumie fedha kuhakikisha kwamba ndio utakaotoa mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM 2015 alisema. Alitahadharisha kuwa ikiwa wanatumia mamilioni ya fedha ili kumpata mgombea, maana yake ni kwamba wanaotoa fedha hizo za rushwa, wanawekeza ili baadae wapate faida kubwa. Hivyo aliwataka wakazi wa Bagamoyo kutokubali hali hiyo, vinginevyo watamalizwa kiuchumi. Prof. Lipumba alisema kuwa kugundulika kwa gesi nyingi nchini, mafuta na uranium imekuwa kichocheo kikubwa cha watu kuamua kutumia kila njia kuhakikisha kwamba wanaingia madarakani. Lengo ni kwenda kufaidi mapato ya rasilmali hizo muhimu kwa maendeleo ya nchi, ambazo zinatarajiwa kuliingizia Taifa mabilioni ya fedha siku za usoni. A l i s e m a Ta n z a n i a imebarikiwa kuwa madini ya kila namna, dhahabu, almasi, huku katika maeneo ya Tunduru na Dodoma yakigunduliwa madini ya uranium, ambayo hutumika kwa ajili ya kufua umeme na kutengeneza silaha nzito. Alitoa mfano kwamba
litakalotokana na gesi kufuatia utafiti uliofanyika katika nchi za Mexico, Brazil na Indonesia. Alisema utafiti huo umebaini kuwa njia nyepesi ya kumsaidia mwananchi maskini aondokane na umaskini wake, ni kumkabidhi fedha taslim. Watu maskini wanapopata kipato hutumia vizuri fedha zao ili kuboresha maisha ya familio zao. Vile vile watu maskini wana vipaji vya ujasiria mali unaochochewa na hali zao. Lakini tatizo kwao hawana mitaji. Ikiwa watapata fedha taslim, watapata mitaji na wataweza kuanzisha shughuli zao za kibiashara na kujiajiri. Alisema Prof. Lipumba. Alifafanua zaidi kuwa njia ya kuwapatia watanzania fedha taslim zitakazotokana na pato la rasilmali za nchi yao ni rahisi. Alisema kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya vitambulisho vya uraia vinavyotumia alama za mwili, kila mtanzania anaweza kukiwa na fedha hizo. Alisema nchini India, kuna watu bilioni moja na milioni mia mbili, ambapo umewekwa utaratibu wa kutoa vitambulisho kwa raia kwa kutumia alama za mwili. Kwamba mtu anapigwa picha katika mboni ya jicho na kuchukuliwa alama za vidole, viungo ambavyo alama zake hazifanani hivyo kuwa rahisi kuwatambua watu wanaostahili kupata mgawo huo wa serikali. Aidha alisema teknolojia ya simu imekuwa njia rahisi zaidi kuwapatia watu fedha. Alisema iwapo serikali itaweka utaratibu wa akaunti ya benki kwa njia ya simu za mkononi kwa kila mtanzania, ni rahisi kumpatia raia huyo mgao wake kwa kumwekea kwenye akaunti yake na kwamba hilo linawezekana. Hata hivyo aliendelea kuitupia
Inaendelea Uk. 4
4
Na Mwandishi Wetu MHESHIMIWA Amani karume anataka Wazinzibari wanaotaka serikali tatu nao wasikilizwe. Mimi nakubaliana naye 100%. Hata hivyo inaonekana kuwa kuna watu imewakera sana, hasa CCM wahadhina. Karume alisema, kuhusu katiba mpya Watanzania wote na Wazanzibar pia wasikilizwe na watoe maoni yao hata yale tusiyoyapenda. Akaendelea kusema kwamba, kuhusu Muungano wapo wanaotaka serikali mbili wasikilizwe, wapo wanaotaka muungano wa mkataba wa serikali mbili- wasikilizwe na wapo wanaotaka serikali tatu wote wasikilizwe. Aliposema muungano wa mkataba kelele zilianza, aliposema serikali tatu kelele ziliongezeka. Wapiga kelele hawakuwa na ujasiri wa kumzomea lakini walionekana kupiga kelele za kutokubaliana naye kwa kuwa hawakufanya hivyo kwa wasemaji wengine ni dalili za wazi kwamba aliwakera wengi. Japokuwa magazeti hayakuandika kwa upana habari hiyo, hotuba ile imefungua ukurasa mpya kuelekea serikali tatu ambayo ni Sera ya Chadema na CUF muungano wa serikali mbili sasa ni njia panda. Kabla ya kukia hoja hiyo, Amani Karume aliwakubusha wajumbe kuhusu Chama cha ASP, akawaonesha wajumbe kadi yake ya uanachama wa ASP na kuwasomea malengo ya ASP yaliyoko
Habari
AN-NUUR
Inatoka Uk. 3
lawama serikali ya CCM, kwamba imeshindwa kuwa na mipango ya kukuza uchumi na kuongeza ajira nchini. Alisema Tanzania ina bahati ya kijiografia, inapakana na bahari, kuna ardhi inayokubali kila aina ya mazao, kila aina ya matunda, lakini leo Bagamoyo ambayo ni maarufu kwa zao la mananasi na maembe, miaka hamsini baada ya uhuru hakuna walau japo kiwanda cha kusindika matunda, zaidi ya kuozea mashambani. Bagamoyo matunda yanakubali, mananasi yanakubali, maembe yanakubali, kwa nini miaka hamsini baada ya kujitawala bado juisi ya embe, nanasi, passion inatoka nje ya nchi. Tumeshindwa hata kuweka kiwanda cha kusindika matunda
kutatanisha, kijana huyo alifikishwa mahakamani hapo pamoja na Haruna Ahadi, muuza duka ambaye ndiye Juzuu aliyokuwa akiisoma, aliporwa na kukojolea.
Habari zinaeleza kuwa kijana Ahadi, anashikiliwa kwa madai kuwa kwa kiasi fulani alichochea mwenzake kukojolewa Juzuu yake. Kesi hiyo haikutajwa mahakamani hapo kwa kuwa hakimu aliyepangwa kuisikiliza, Mh. Dudu, hakuwepo mahakamani akidaiwa kuwa amesafiri, hivyo mtuhumiwa kurudishwa rumande hadi Novemba 29 kesi yake itakapotajwa tena. Siku ya Jumamosi mwezi uliopita, Daud Kapaya,
kampuni ya Agritanza Ltd, kupitia mkataba ulifanyika Juni 18, 2011. Kufuatia maombi ya wakili wa watuhumiwa, Jamhuri kuahidi kuwa Sheikh Ponda hatokuwa na pingu pindi anapokuwa mahakamani hapo. Kwa upande mwingine Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Bw. DPP Eliazer Feleshi, alileta pingamizi la dhamana kwa Mukadamu na Sheikh Ponda akidai kuwa usalama na maslahi ya Jamhuri yataadhiriwa ikiwa mtuhumiwa huyo atakuwa nje kwa dhamana. Sheikh Ponda Issa Ponda na Bw. Mukadam Abdallah Saleh, walirejeshwa rumande baada ya dhamana zao kuendelea kufungwa hadi hapo kesi yao itakapotajwa Novemba 29 mwaka huu.
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
Mitambo ya Aliyemtukana Muhammad nyuklia Iran (saw) aenda jela kuanza kazi
TEHRAN Mkuu wa Taasisi ya Nishati ya Nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Fereydun Abbasi, amesema kuwa katika kipindi cha miezi michache ijayo, shughuli za awali za mitambo ya nyuklia iliyopo Bushehr, kusini mwa Iran zitafunguliwa rasmi. Fereydun Abbasi, amesema mitambo hiyo ya nyuklia ya Bushehr itafunguliwa Januari au Februari mwakani na wataalamu wa Irani baada ya kufanyika majaribio kadhaa ya kitaalamu. Ameongeza kuwa kazi za wakandarasi wa Kirusi zinafikia ukingoni na kilichobaki ni kukabidhiwa rasmi wataalamu wa Iran kuiendesha mitambo hiyo. Abbasi amesema hivi sasa mitambo ya Bushehr ina uwezo wa kuzalisha megawati 1000 za umeme, ambapo kiwango hicho kitaongezwa hadi kukia megawati 4000 hadi 6000 na hatimaye kuingizwa kwenye gridi ya taifa.
LOS ANGELES MAHAKAMA nchini Marekani imemhukumu yule mtu aliyetengeneza filamu ya kuwatukana Wa i s l a m u n a M t u m e Muhammad (saw) kwenda jela baada ya kukutwa na hatia ya kuvunja amri ya mahakama ya kutofanya uhalifu kwa kipindi cha miaka minne ikiwa ni sehemu ya hukumu kufuatia kutiwa hatiani kwa kufanya wizi katika benki siku za nyuma (breaching his probations terms). Mark Basseley Youssef, mwenye umri wa miaka 55, ambaye alitengeneza na kuongoza filamu iliyozua vurugu kufuatia maudhui yake ambayo yanamtusi Mtume Muhammad (saw) na Waislamu kwa ujumla, atatumikia kifungo chake katika gerezani (US federal prison) baada ya kukiri makosa manne aliyotuhumiwa nayo ya kutumia vitambulisho feki. Makosa hayo yanakiuka hukumu ya adhabu aliyopewa siku za nyuma ambapo alikutwa na hatia ya kuiba kitapeli katika benki mwaka 2010. Youssef ni mhusika mkuu wa filamu inayokashfu Uislamu na kuzua maandamano makubwa sehemu mbalimbali duiniani, ambapo makumi ya watu walipoteza maisha katika wimbi hilo la maandamano. Filamu hiyo pia ilisababisha tukio la shambulio la S e p t e m b a 11 , a m b a p o
Balozi mdogo wa Marekani nchini Libya Chris Stevens, aliuliwa Benghazi pamoja na wamarekani wengine watatu.
Balozi mdogo wa Marekani nchini Libya Chris Stevens, aliuliwa Benghazi pamoja na wamarekani wengine watatu. Mwezi Februari 2009, mahakama iliwatia hatiani Youssef na wenzake kwa kuiibia benki kwa njia za udanganyifu kwa kutumia utambulisho na namba za usalama za wateja katika matawi ya benki ya Wells Fargo California na kutoa kiasi cha dola 860 katika kaunti za wateja hao. Alifungwa jela miezi 21 na kuamriwa kutotumia komputa au Internet kwa kipindi cha miaka mitano, vinginevyo ni mpaka apate kibali maalum. Pia alipigwa
marufuku kutumia majina ya kisanii wakati akitumikia adhabu yake ya kuwa chini ya uangalizi baada ya kumaliza kifungo cha jela. Alikamatwa Septemba na kushtakiwa kwa kuvunja vipengele vinane ya adhabu ya uangalizi iliyokuwa ikimkabili. Mwezi uliopita alikana tuhuma zote lakini wiki hii amekubali makosa manne huku mengine manne yakiondolewa. Jaji wa Mahakama (District Judge), Christina A Snyder, alisema kuwa Youssef, ambaye tayari ameshakaa rumande kwa wiki tano, atatumikia miezi 12 jela kufuatia kuvunja amri ya kuwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha miaka minne.
PHINON PEIN Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay, ameitaka serikali ya Myanmar kuwapa haki za kiraia Waislamu nchini humo. Bi. Navi Pillay, ambaye alikuwa akihutubia katika Mkutano wa Kimataifa wa Demokrasia huko Bali, Indonesia amesema serikali ya Myanmar inapaswa kuchukua hatua za kuwapa haki za kiraia Waislamu wa kabila la Rohingya na kuishi nao kwa uadilifu. Aidha nchi hiyo kubadili sheria zake za sasa na kuwaruhusu Waislamu kuwa na haki ya uraia. Pillay amesema Umoja wa Mataifa una wasiwasi mkubwa kuhusu ukandamizaji na juhudi zinazofanywa nchini Myanmar kwa ajili ya kuangamiza jamii ya Waislamu wa Rohingya. Shauri la Umoja wa Mataifa la kutaka kupewa uraia Waislamu wa Myanmar limetolewa siku moja tu baada ya wanaharakati wa haki za binadamu wa kimataifa kutoa wito wa kupelekwa askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Myanmar ili kukomesha ukandamizaji na mauaji yanayofanywa dhidi ya Waislamu magharibi mwa nchi hiyo. Katika hatua nyingine, shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International, limeituhumu serikali ya Ethiopia kuwa inafanya ubaguzi dhidi ya Waislamu nchini humo. Amnesty International imetoa tuhuma hizo kutokana na mwenendo wa serikali ya Addis Ababa wa kuwatia nguvuni Waislamu kwa kosa lililotajwa kuwa ni kushiriki kwenye maandamano ya amani ya kudai uhuru wa kidini.
DOLA za Kimarekani
6
Na Omar Msangi, Hebron
Makala
AN-NUUR
Makala
AN-NUUR
Nabii Ibrahim) unaokisiwa kujengwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Tunaruhusiwa kupita katika upenyo wenye mashine za usalama (security) za ukaguzi na kutokezea kwenye uwazi ambapo kwa mbele kiasi meta 300 tunaona Msikiti wa Nabii Ibrahim. Lakini tunaposogea mbele tunakuta ukuta wa Polisi harakaharaka wanafunga njia ya kupita. Huu ni Msikiti w a Wa i s l a m u , l a k i n i wanatuzuiya kuingia, unaona Waisrail wale wanaingia, wamegeuza Msikiti huu ni hekalu lao, anaeleza mmoja katika wenyeji wetu. Kwa mbele tunaona Waisrail waliovaa vile vibandiko vya dini ya Kiyahudi wakipanda ngazi kuingia na kwa upande mwingine tunaona mabasi ya Wayahudi yakirudi na watu ambao tayari washaingia msikitini humo sasa wanaondoka. Tulisimama hapo kwa muda tukipewa maelezo juu ya Msikiti huo, lakini kubwa tukifahamishwa kuwa mpaka mwaka 1994 Msikiti huo ulikuwa chini ya mikono ya Waislamu. Wenyeji wakiswali hapo na watu kutoka nchi mbali mbali wakija kuutembelea. Lakini mwaka 1994 ilikuwa katika swala ya Subhi mwezi wa Ramadhani, Msikiti umefurika Waislamu wakifanya ibada, aliingia askari mmoja wa Kiyahudi na silaha akauwa Waislamu wengi na kujeruhi mamia. Kutoka siku hiyo, kwanza eneo lote linalozunguka msikiti likawekwa amri ya kutotembea na shule zikafungwa kwa miezi mitatu. Baadhi ya nyumba na shule jirani na hapo zikachukuliwa na kugeuzwa kuwa makazi na shule za Kiyahudi. Waislamu wakapigwa marufuku kuingia katika Msikiti huo. Baadae serikali ya Israil ikadai kuwa Israil ndio yenye haki zaidi na Msikiti huo. Kwa hiyo wakatenga sehemu ambayo watakuwa wanaruhusiwa Waislamu kuingia na sehemu kubwa kuwa ni ya Waisrail. Lakini hata hiyo sehemu ambayo inaambiwa kuwa ni ya Waislamu nayo mtu hawezi
kuingia muda wowote atakao mpaka aruhusiwe. Vinginevyo marufuku kama sisi tulivyozuiwa. Baada ya kuwa tumekwama kuingia Masjid Ibrahim, tukashika njia nyingine kuangalia nyumba za Wapalestina na shule zao ambazo zimetaishwa na kupewa Walowezi wa Kiyahudi na kwamba ni marufuku kwa Mpalestina kupita mtaa huo. Unaona nyumba ile mimi nimezaliwa na kukulia pale, hivi sasa ni marufuku, siruhusiwi japo kukaribia nyumba yetu. Mimi nimesoma shule ile pale hivi sasa ni shule ya Kiyahudi tena inasomesha Wayahudi hawa wa siasa kali. Anasimulia mwenyeji wetu mmoja huku akituonyesha kwa kidole majengo hayo ambayo yapo kama mita 100 hivi kutoka pale tuliposimama. Msikimbie, msiogope, msiwaone wana bunduki nzito lakini wanatuogopa, sisi tunawaambia sisi sio magaidi, sisi hatuwachukii Wayahudi, hatuwachukii askari wa Israil, tunachotaka ni utu wetu, tuishi kama binadamu kama manavyoishi nyinyi askari, tunataka tubaki Wapalestina na ubinadamu wetu, sisi ni binadamu, oneni wenyewe ile ni nyumba yetu, ile ilikuwa ndio shule niliyosoma miaka ya 1980/90s, leo siruhusiwi kupita mtaa huu, anasema kijana mmoja. Anayasema hayo huku askari wa Israel, hata walipotokea hatujui, wametuzingira mbele na nyuma, mbele hatuwezi kwenda maana wamesimama askari wasiopungua 20 na silaha nzito. Nyuma nako wapo wengi na silaha na magari mawili ya polisi. Barabara haipitiki tena. Ilibidi turuke uzio wa barabara kuna kiuchochoro tukawa tunapita mpaka tukaka kwenye njia tuliyojia ya kupita Masjid Ibrahim kuelekea tulipotoka. Hata hivyo, katika wenyeji wetu wale, hakuna aliyekimbia. Ndio kwanza wakawa wanaimba kwa nguvu nyimbo za kuhamasishana kudai ardhi yao na haki zao. Ilikuwa ni kishindo cha sauti
WAANDISHI wa habari kutoka nchi mbalimbali wakiwa Palestina. Wa m e n i k u m b u k a ya hamasa na kuilani Israil kuwa kila aliyekuwepo wanamnasa na kumuingiaza maana mimi muda mwingi hali iliyotufanya hata wale nimekuwa katika jela za wageni ambao walikuwa katika kumbukumbu zao. Walitusindikiza kwa Israel na nadhani maisha washaingiwa na woga nyuma na mitutu yao hadi yangu yote yatakuwa hivi, kupata mdadi. Kwa wengi lilikuwa tulipoka lango la kutokea haya ndiyo majaaliwa yetu, tukio la aina yake. Kwa huku wakituhimiza kufanya lakini hatutakata tamaa muda hiyo waandishi wa habari haraka. Wakati tunafika wa kuwa tupo hai tutapigania kutoka sehemu mbalimbali katika kituo cha ukaguzi
duniani ambao walikuwepo, ilikuwa hekaheka, sio ya kukimbia risasi, bali angalau kupata picha. Lakini wakati waandishi wanapigana vikumbo na kamera zao, askari wale nao baadhi yao walikuwa na kamera za video na wao wakihakikisha
kilichojaa polisi, mmoja akamwita mmoja wa wenyeji wetu ambaye nilikuwa nikiongea naye. Wakachukua muda kama dakika mbili tatu. Aliporudi namuuliza nini walikuitia akaniambia kuwa walimkumbuka ndio wakawa wanamhoji.
haki yetu ya kutambuliwa kama binadamu walio na haki ya kuishi kwa heshma na utu kama binadamu wengine. Alieleza huku tukisukumwa kuharakisha kuondoka nje ya eneo la kuingilia Masjid Ibrahim.
8
Biamillaahi naanza, kwalo jinale JALILI, Kisha ninaandiliza, kwa swala yake RASULI, Ridhwani nafwatiza, kwa swahabaze RASULI, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. MOJA NNE TATU TATU, hatunao ikhiwani, KUBWA sote sasa kwetu, ni kufanya TATHMINI, Tuchungue mambo yetu, pamwe na ya dini yetu, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. RISALA nawatumia, wa Bara na Visiwani, KAMBA tunoungania, ni MOJA ulimwenguni, Kamwe sitowabania, kwani nyote ikhiwani, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Iwakie Unguja, kadhalika nako Pemba, Sisapoti Uunguja, bali hata na Upemba, DINI yetu ndio HOJA, sote inayotupamba, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Biamillaahi naanza, kwalo jinale JALILI, Kisha ninaandiliza, kwa swala yake RASULI, Ridhwani nafwatiza, kwa swahabaze RASULI, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. MOJA NNE TATU TATU, hatunao ikhiwani, KUBWA sote sasa kwetu, ni kufanya TATHMINI, Tuchungue mambo yetu, pamwe na ya dini yetu, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. RISALA nawatumia, wa Bara na Visiwani, KAMBA tunoungania, ni MOJA ulimwenguni, Kamwe sitowabania, kwani nyote ikhiwani, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Iwakie Unguja, kadhalika nako Pemba, Sisapoti Uunguja, bali hata na Upemba, DINI yetu ndio HOJA, sote inayotupamba, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Sasa narejesha Bara, baada ya Visiwani, Nabtadi na Tabora, kisha Kigoma na Pwani, Kadhalika na Mtwara, Lindi na nyote kusini, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Kagera hadi Arusha, Dar na Kilimanjaro, Kote RISALA narusha, hadi kule Morogoro, Sitaki kuahirisha, au kuweka kiporo, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA.
Makala
AN-NUUR
BINADAMU tunatakiwa kufahamu kusudi la Mwenyezi Mungu (Allah sw) kutuumba. Inatupasa kutambua lengo la maisha yetu hapa duniani na ahera tuendako. Mwenyezi Mungu muumbaji kutulipa kile alichokusudia, inategemea zaidi tumefanya nini hapa ardhini (duniani). Kama tumefanya uovu, tutalipwa kutokana na uovu. Malipo ya uovu bila
shaka ni adhabu kali. Kama tutafanya mema, basi mema hayo yatatusaidia kwenda peponi. INSHAALLAH. Kutokana na picha hapo juu, naomba Waislamu tuandike Insha isiyozidi maneno (250) kwenda gazeti la Annuur, somo kuu likiwa linahusu Unaelewa nini kuhusu kaburi ukiwa kama Muislamu. NB: Uongozi wa Ann-uur
naomba mnisaidie kuitoa barua hii kama ombi la Insha kwa waumini kupitia gazeti letu. Rashidi Idrisa Tindwa (BA Education rst year 2012) +255753071185, +255715416490 C H U O C H A W A I S L A M U MOROGORO.
SHULE YA SEKONDARI YA BONDENI NAFASI ZA KIDATO CHA KWANZA KWA MWAKA 2013
UONGOZI WA SHULE UKISHIRIKIANA NA JUMUIYA YA WANATAALUMA WA KIISLAM TANZANIA (TAMPRO) WANAYOFURAHA KUWATANGAZIA WAZAZI NA WALEZI KUWAHI NAFASI ZA KIDATO CHA KWANZA. AIDHA NAFASI ZIPO KWA WALE WOTE WANAOTAKA KUHAMIA KATIKA KIDATO CHA PILI, TATU, NNE, NA TANO. TUNAO WALIMU WENYE SIFA NA MAKINI WATAKAOHAKIKISHA KUWA MWANAO ANAPATA ELIMU BORA NA MALEZI MEMA USAILI WA KUJIUNGA NA SHULE UTAFANYIKA TAREHE 30/11/2012 KATIKA ENEO LA SHULE SAA TATU ASUBUHI. DARASA LA QT NA PC LITAKUWEPO MASOMO YATAANZA MWEZI WA KUMI NA MBILI MWAKA 2012. GHARAMA YA FOMU NI TSHS.10, 000 KWA MAWASILIANO: SIMU NO.0754 673327 SIMU NO.0787 754244/0715 754244. WABILLAH TAWFIQ. IMETOLEWA NA UONGOZI WA SHULE- TAMPRO. S.L.P.2013, ARUSHA
RISALA kupeperusha, hino nayo ni IBADA, Dodoma napeperusha, Tanga, Manyara, Singida, Rukwa sitajiepusha, kutimiza hii ada, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Mara nakukumbukeni, kadhalika na Shinyanga, Nyote kwangu majirani, aula mkaniunga, Mwanza sikusahauni, na ndiko natia nanga, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Kadi tama nimeka, mwisho wa RISALA yangu, LENGONI sote kuka, ndo hasa shauku yangu, Na nilipoghalika, nisamewe kosa langu, SOTE TUJITATHMINI, KWA YA MWAKA ULOPITA. Abuu Nyamkomogi Mwanza
Makala/Tangazo
AN-NUUR
Na Shekh Mustafa Rashad Rushdy Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu peke yake na rehema na amani zimfikie yule ambaye hakuna Mtume baada yake, na ninashuhudia kuwa hakuna Mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu tu. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu, hakika yetu tumekutuma uwe ni shahidi na mtoa biashara na muonyaji na ili mumuamini Mwenyezi Mungu asubuhi na jioni Surat Fath, aya ya 8 9. Heshima na utukufu ni wa Mwenyezi Mungu, yeye ni mtukufu na yeye ndio mkubwa, yeye ndiye mwenye kibri na kuwaheshimu Mitume ni wajibu kwa sababu wao wamehifadhiwa na kufanya makosa, na kuwaheshimu wakubwa na kuwahurumia wadogo ni jambo la lazima na katika hadithi tukufu inaeleza kuwa (si mwenzetu kwa yule asiyewaheshimu wakubwa na asiyewahurumia wadogo na asiyehifadhi heshima ya wanachuoni wetu. Bali Mtume (S.A.W) amembashiria mwenye kumkirimu mkubwa kwa ukubwa wa umri pale aliposema, (hamkirimu kijana, mtu mzima isipokuwa naye atampatia heshima na kuheshimu ni alama za wenye akili, na yule aliyepewa akili utamuona ni mwenye heshima katika maneno yake na mwendo wake na kukaa kwake na kazi zake. Mtume (S.A.W) ana mifano bora ya heshima pale aliponyenyekea na pale alipokuwa mbora wa watu kwa unyenyekevu, yakawa maisha yake ni ya wastani na vyakula vyake vyepesi na godoro lake ni vitambaa, pamoja na hayo yote alikuwa na utisho wake kwa watu. Hebu kumbuka pale alipoingia mwarabu mmoja kwa Mtume (S.A.W) ikaanza kutetemeka miguu yake na mwili wote kwa ujumla,
ndipo Mtume (S.A.W) akamwambia mwarabu yule kuwa, Itulize nafsi yako kwa hakika mimi ni mtoto wa mwanamke ambaye alikuwa akila vyakula hata vile vya kawaida tu katika mji wa Makka tukufu. Alikuwa Mtume (S.A.W) katika vita vya badri pamoja na Abi Lubaba na Sayed na Ally Bin Twalib, wanapokezana ngamia mmoja. Akasema Ally na Abi Lubaba hebu tushindane mwendo na mimi nitajiri sana wa kulipa wengi. Tujue kuwa heshima sio kiburi na kudharau watu na kujikweza na kuwabagua wengine. Bali heshima ni kumuheshimu wa mbali na wa karibu na unayemjua na usiyemjua, na kumpa kila mwenye haki haki yake na muongozo wa Uislamu ni kutokumdharau mwingine. Na Mitume yote ilikuwa midahalo yao ni kwa kutumia hoja na heshima na upendo na alikuwa kila Mtume akihojiana na watu wake kwa kusema, Enyi watu wangu, hii ni kwa utukufu na heshima. Na mtu mwenye heshima ni yule mwenye kuheshimu wengine na kuwaweka watu sehemu zao, na inapopotea heshima na upendo pia hupotea. Na hapo ndipo mwenye nguvu humla mnyonge na tajiri humla masikini na (Rais) humla raia (kiongozi humla anayemuongoza. Heshima haishii kwa kiongozi na anayeongozwa, huu ni uelewa nyu. Heshima ni muhimu hadi katika familia kama vile mume na mke pamoja na watoto wake. Hili ni daraja la wote kati ya viumbe wote. Na katika hadithi (yule ambaye asiyemshukuru Mwenyezi Mungu hawezi kuwashukuru watu, na kuvitukuza viumbe vya Mwenyezi Mungu ni miongoni mwa kutekeleza amri zake. Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu, Mmekuwaje hamuweki heshima ya Mwenyezi Mungu, na hali yeye amekuumbeni namna baada ya namna Surat Nuuh aya ya 13 na 14.
NAFASI ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO UALIMU WA MAARIFA YA UISLAMU KWA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI - 2013
Tunachukua fursa hii kuwatangazia Waislamu wanaume na wanawake nafasi za mafunzo ya Ualimu wa Maarifa ya Uislamu kwa shule za Msingi na Sekondari yatakayoanza Februari 2013. SIFA NA MASHARTI YA KUJIUNGA Muombaji atimize sifa na masharti yafuatazo:(i) Awe amemaliza juzuu ya 1 na 2 ya Maarifa ya Uislamu Darasa la Watu wazima kabla ya kujiunga. (ii) Awe amehitimu darasa la saba au kidato cha nne na awe anafundisha Madrasa au Maarifa ya Uislamu katika kipindi cha dini shule za Msingi au Sekondari kwa muda usiopungua mwaka mmoja. (iii) Awe anajua kusoma Quran kwa ufasaha. FOMU ZINAPATIKANA CHUONI UBUNGO KWA GHARAMA YA SHILINGI ELFU TANO TU. MUHIMU Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 30/11/2012. Usaili utafanyika siku ya Jumamosi tarehe 01/12/2012 saa 2 asubuhi. Wabillah Tawiq MKUU WA CHUO
10
Habari
AN-NUUR
SERIKALI imetakiwa kuyapa uzito malalamiko ya Waislamu kuhusu mali za Waislamu zinazouzwa na Taasisi ya BAKWATA, kwa kuwa mali hizo ni Waqfu na hazipaswi kuuzwa. Hayo yamesemwa na Maalim Ally Bassaleh, akiongea na Waislamu mara baada ya swala ya Ijumaa wiki iliyopita, katika Msikiti wa Idrisa, Kariakoo, Jijini Dar es Salaam. Kauli hiyo ya Maalim Bassaleh imekuja baada ya kujiri matukio ya hivi karibuni yaliyosababisha kukamatwa na kufunguliwa mashtaka baadhi ya Waislamu. Alisema mali yoyote ya Waqfu iliyo chini ya Bakwata katika nchi hii, ni mali ya Waislamu na kwamba Bakwata au taasisi nyingine yoyote au kiongozi wa Kiislamu hana haki wala sheria ya kuuza mali za Waqfu kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu. Serikali inapaswa kuangalia kwa kina malalamiko ya Waislamu dhidi ya Bakwata, sio kuwasulubu wanaolalamika kwa nguvu za dola na kuwavumishia sifa mbaya. Inapaswa kuangalia chanzo cha malalamiko ya Waislamu na kutafuta ufumbuzi Ili kuepusha migongano na kuuzwa holela mali za Waislamu ambazo nyingi ni waqfu. Alisema Maalim Bassaleh. Alisema kuwa hata kama zitakuwepo sababu za kujaribu kuhalalisha uuzwaji wa mali hizo, bado zitakuwa hazina msingi wowote kwa kuwa mali hizo ambazo nyingi ni nyumba na viwanja, ni rasilmali ambazo Waislam na kila taasisi ya Kiislamu inahitaji kumiliki kwa maelendeleo ya jamii husika na si kuuza. Alisema Bakwata ilimilikishwa m a l i n y i n g i z a Wa i s l a m u zilizokuwa chini ya iliyokuwa Jumuiya ya Waislamu ya Eat Africa Muslim Welfare Society (EAMWS) iliyovunjwa na Mwalimu Julius Nyerere, hivyo Bakwata ilipaswa kuzisimamia kwa uadilifu na kusaidia Waislamu na Uislamu kupiga hatua kimaendeleo, kuliko ilivyo sasa ambapo sehemu kubwa ya mali hizo zimeuzwa na nyingine kukodishwa kwa hasara. Alisema licha ya kuuza mali za Waislamu, Bakwata badala ya kuwaunganisha Waislamu, limekuwa baraza linalotumika kinamna kuwagombanisha Waislamu wenyewe kwa wenyewe na kuwafanya Waislamu wasiwe na maelewano. Akitoa mfano wa sakata la kiwanja cha Markazi Changombe, alisema waliouza ni taasisi ya Kiislamu (Bakwata) walionunua ni Waislamu, na wanaojaribu kukinusuru kuuzwa ni Waislamu. Aliongeza kuwa kwa sababu ya kugonganishwa huko, hata walioshitakiwa hawakushtakiwa na Bakwata wala na anayedawa kununua kiwanja hicho, bali
Maalim Ally Bassaleh. imekuja baada ya kuwepo zoezi walioamua kusilimu Alisema kwa vijana wa Kiislamu kila siku Maalim Bassaleh. asubuhi hupita mahospitalini, Alisema hata katika kadhia hususani katika hospitali za ya hivi karibuni, Maaskofu Temeke, Kinondoni na Ilala, walikwenda mbali zaidi kwa wakitoa misaada ya hali na kuwataka Wakristo kuyalinda chakula kwa wagonjwa bila makanisa yao kwa mishale, kubagua dini zao. mikuki, visu, mapanga na mbo Alisema hata yeye (Bassaleh) ili kupambane na Waislamu. amekuwa akishiriki katika kutoa Alisema kama kweli kauli hiyo huduma hizo katika hospitali ya imetoka kwa viongozi hao, Ocean road, Jijini Dar es salaam. huo ni uchochezi na ni kauli ya Mbali na huduma nyingine, kuhatarisha amani miongoni lakini pia hufanywa usa katika mwa wananchi lakini hakuna hospitali hizo kama sehemu aliyekamatwa. ya huduma wanazozifanya Alihoji kama mameno hayo Waislamu hao wakapo katika yangesemwa na Sheikh wa hospitali hizo. Kiislamu, akanadi Msikitini Baadhi ya wagonjwa huamua kwamba Waislamu wajiandae kusilimu wenyewe kwa hiyari kwa visu, mapanga, mishale yao baada ya kufanyiwa wema kulinda Miskiti yao na wala na makundi hayo ya Kiislamu. asiwataje anaokusudia kupamba Sasa hilo la kusilimu ndio nao, sheikh asingeka siku ya limekuwa karaha kwa Maaskofu pili bila kukamatwa. na sasa wanakuja na kauli za lakini huyu anayesema tna. Taarifa zilizopo hivi sasa, wazi tujiandae kupambana na wanakaria wagonjwa mia moja Waislamu, hashughulikiwi.
Msikiti wa KIBUTA- Kitondwe B Munga- Kisarawe Wanaomba Msaada wa Kuchimbwa KISIMA cha Maji. Kwa Mawasiliano Piga No. 0656 092 436 au 0685 171 221
11
Habari
AN-NUUR
wa Misri, Gamal Abdel Nasser, iliahidi kujenga Chuo Kikuu cha Kiislamu nchini na kubainisha kuwa ahadi hiyo bado ipo kwa kuwa yalikuwa ni makubaliano ya kimaandishi kati ya serikali ya Tanzania na Misri. Dkt Osama alisema, pamoja na kwamba ni miaka mingi imepita sasa, lakini kila kitu kinakwenda kwa mipango. Alisema mipango hiyo kwa sasa ipo katika mchakato kwa kuwa serikali ya Misri inakusudia kutekeleza ahadi ya kuleta Chuo Kikuu cha Kiislamu Afrika Mashariki. Kila kitu kina mipango yake, hivi sasa kuna mipango ya kuleta Chuo Kikuu cha Kiislamu watakachosoma Watanzania na watu wa Afrika Mashariki. Chuo kitafuata muongozo wa Chuo Kikuu cha Al-Azhar Sharif cha Cairo, Misri. Alisema Mkuu huyo wa Chuo. Akifafanua kuhusu unyu wa ardhi kufuatia kumegwa na kuuzwa sehemu kubwa ya eneo lililotengwa hapo Changombe, huku kukiwa na mchakato wa kuamsha kra za kujenga Chuo Kikuu katika ardhi hiyo kama ilivyokusudiwa miaka 44 iliyopita, alisema ikiwa haitatosha watalazimika kuiomba Serikali ya Tanzania iwapatie eneo jingine litakalokidhi haja. Alisema Chuo hicho kitagharamikiw a na na Serikali ya Misri kuanzia ujenzi na uendeshaji wake. Kama ardhi haitatosha basi tutakuwa tayari kuiomba Serikali ya Tanzania itupatie ardhi ili tuweze kujenga hicho Chuo Kikuu kama ilivyokusudiwa awali. Alisema Dkt. Ismail, akionyesha kusikitishwa na suala hilo. Alisema lengo lao la kujenga uzio katika eneo hilo la Markaz, lilikuwa ni kuhifadhi ardhi hiyo ili kuweza kutekeleza lengo lililokusudiwa kama jiwe la msingi linavyoonyesha kuwa hicho ni Chuo Kikuu Cha Kiislamu. Alisema kwa kuwa katika chuo hicho kwa sasa wanatoa elimu ya dini katika ngazi ya awali, Msingi na Sekondari, sasa walipenda Chuo Kikuu kianze au kiwe hapo hapo. Kuhusu nani mwenye mamlaka ya eneo la Markaz, alisema hapo kuna maswala mawili, kwanza ni kuhusu jengo la chuo lililopo kwa
BAADHI ya viongozi wa Markaz Chang'ombe wakionesha sehemu zilizoharibiwa kufuatia uvamizi uliofanywa na jeshi la polisi Chuoni hapo hivi karibuni. sasa, ambalo limejengwa na kutafuta msaada wa kujenga na Makamu wa Rais wa Rai Misri na wao ndio wasimamizi chuo Kikuu Cha Kiislamu na wa Misri (Sharbasy) kwa na waendeshaji wa chuo kuanzisha uhusiano na nchi niaba ya Serikali yake. hicho. Ama upande wa ardhi, za Kiislamu. Baada ya makubaliano alisema kuna wasimamizi Gamal Abdel Nasser, hayo (1964), Serikali ya Misri wake na jukumu lao ni kutoa akiwa Rais wa Misri wakati iliahidi kujenga Chuo Kikuu ambacho ilikuwa taarifa Polisi, na Ubalozi huo, alimuagiza Makamu cha Kiislamuna kuendeshwa kimilikiwe wa Misri kama kunatukio wake Sharbasy, afanye na EAMWS. Hata hivyo lolote. makubaliano na mikataba na Jumuiya hiyo ilivunjwa na Mwaka 1964, ujumbe EAMWS kwa niaba yake. Rais wa awamu ya kwanza wa iliyokuwa Jumuiya ya Serikali ya Misri ilikubali wa Tanzania (Julius Nyerere) Waislamu waAfrika Mashariki kugharamia ujenzi wa chuo baada ya ujumbe huo kurejea (EAMWS), chini ya Sheikh hicho. Hatimaye Mkataba wa kutoka katika ziara za nchi Hassan bin Amir, pamoja na makubaliano ukatiwa sahihi za Kiislamu na badala yake wazee wa TANU, ulifanya Mjini Cairo kati ya Tewa Said Waislamu waliwaundiwa ziara katika nchi za Kiislamu Tewa, kwa niaba ya EAMWS BAKWATA.
athari kubwa kuliko wengine. Alisema Sheikh Yusuph. Kwa upande wa walimu, Sheikh Yusuph alisema kuwa wao ndio warithi wa Mtume (saw) katika kazi hiyo. Mwalimu kwa mwanafunzi anatakiwa kuzungumza lugha inayofaa,
Anahitaji msaada
kujiendeleza zaidi kwani ndio kwanza safari ndefu ya kusoma inaanza. Jumla ya wahitimu 38 wa kidato cha nne wamehitimu mwaka huu na wale wa darasa la saba wakiwa ni watano. Kwa upande wa shule ya awali ni 23 na ambao wanatarajiwa kuanza darasa la mwakani kwanza (Grade I).
Ommary Abdallah Mketto, ambaye ni mlemavu wa ngozi (Albino) mkazi wa Mtoni Kijichi Dar es Salaam anaomba msaada kumwezesha kufungua biashara ya Stationary. Licha ya kuwa na uwezo wa kufanya kazi, lakini kutokana na ulemavu wake wa ngozi na kutoona vizuri, Mketto amekuwa akikosa ajira kwasababu ya hali yake ya ulemavu. Hivyo ameamua kujiajiri mwenye ili uepukana na maisha ya kuomba na tayari amefanikiwa kusajili biashara yake hiyo No 239430, Ragistration 12 Mach 2010Kijichi Albinism Internet Caf Agriculture katika Manispaa ya Temeke. Msaada anaohitaji kijana huyu ni Mashine ya Photocopy, Printer, komputa na mtaji wa kufungua stationary. Anapatikana Masjid Al Ihyau-Mtoni Kijichi na Masjid Mikocheni Islamic. Kwa mawasilianio zaidi: 0713-376426 au 0784-989860 Wabillah Tawq
AN-NUUR
12
Na Bakari Mwakangwale
JUMUIYA ya Waislamu Sinza, Jijini Dar es Salaam ipo katika mchakato wa kujenga kituo cha huduma za jamii zitakazozingatia maadili na misingi ya Uislamu. Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Shule ya Sekondari ya Luqman, Ustadhi Amin Kinollo, katika mahafali ya tano ya kidato cha nne na darasa la saba katika shule ya Luqman Sekondari na Msingi, mwishoni mwa wiki iliyopita. Ustadhi Amin Kinollo alisema, Jumuiya hiyo kwa sasa inasimamia na kuendesha shule za Awali, Msingi na Sekondari zinazojulikana kwa jina la Luqman Islamic pamoja na Madrasatul- Ikhlas, zilizopo katika Msikiti wa Sinza Palestina, Jijini Dar es Salaam. Alisema katika mipango ya baadaye ya Jumuiya hiyo, ni kujenga Hospitali ambayo itazingatia maadili ya Kiislamu katika kutoa huduma kwa jamii. Ust. Kinollo aliongeza kuwa hivi sasa wapo katika mchakato wa kujenga jengo la ghorofa sita kwenye eneo lao (Plot) namba 936 Sinza Block C, ambalo litakuwa na ofisi za idara mbalimbali ikiwemo maktaba ya Kiislamu, ukumbi wa mikutano pamoja na kidato cha tano na sita. Kwa kutumia ipasavyo ardhi tulizozipata katika maeneo mbalimbali hapa nchini, Jumiya itajenga na kuanzisha Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo vya ujasiria mali kwa vijana na jamii kwa ujumla. Alisema Ust. Kinollo. Alisema pamoja na kuwepo mikakati hiyo, Waislamu na wadau mbalimbali kwa ujumla wanaombwa kutoa michango yao ya hali na mali ili kuweza kukia malengo ya Jumuiya. Aliongeza kuwamoja ya mafanikio yaliyopatikana tangu imeanzishwa Jumuiya hiyo, ni
kwa mwalimu huku asilimia shirini ikitokana na juhudi za mwanafunzi mwenyewe. Wataalamu wanasema katika miaka mitano ya mwanzo ya mtoto anakuwa na uwezo wa kushika vitu kwa haraka. Hivyo mzazi akiwa na kauli zisizo na maadili, motto atshika hayo bila kujua athari zake. Ndio maana tunasema kuwa mzazi ana
Inaendelea Uk. 11
uliotokea c h u o n i h a p o kwa kuvunjwa milango, madirisha na kisha kuibiwa vitu mbalimabali. Taarifa hiyo imeorodhesha vifaa vilivyoharibiwa kuwa ni mashine tatu za x-Ray, Kompyuta tano, Amplifire pamoja na Microphone moja. Taarifa hiyo imedai upelelezi wa shauri hilo bado unaendelea na kwamba, hakuna mali iliyokamatwa wala watuhumiwa. Maelezo hayo kutoka osi ya Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Changombe kupitia barua yenye kumbukumbu namba CHA/ CID/B.I/I/VOL.42/239, yamekuja kufuatia maombi yaliyotumwa kutoka katika kituo hicho kupitia barua ya Inaendelea Uk. 11
BAADHI ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Luqman, wakiwa katika mahafali ya tano ya kidato cha nne na darasa la saba katika shule ya Luqman Sekondari na Msingi, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.