Escolar Documentos
Profissional Documentos
Cultura Documentos
21.12.2016
2
sambamba na tatizo la tabianchi ambalo linapelekea maji kupungua kwa kiasi kikubwa
katika vyanzo vyake.
Pamoja na hayo, Dk. Shein alipongeza hatua za Benki hiyo katika kuiunga mkono
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye sekta ya Mawasiliano ya barabara kwa
Unguja na Pemba ambazo zipo zilikuwa zimemalizika pamoja na zile ambazo
zinatarajiwa ujenzi wake kuanza na nyengine kuendelezwa.
Alieleza kuwa miradi ya barabara kisiwani Pemba itasaidia katika kuendeleza sekta
za maendeleo ikiwemo sekta ya utalii sambamba na juhudi nyengine zinazoendelelea
kuchukuliwa na serikali kisiwani humo ikiwemo uimarishaji wa uwanja wa ndege
ambayo nayo itachangia kukua kwa sekta hiyo ya utalii kisiwani humo.
Aidha, Dk. Shein alisema kuwa mbali ya Benki hiyo kutoa ushirikiano wake katika
kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo hapa nchini zikiwemo maji, barabara,
kilimo, nishati, afya, elimu na utawala bora pia, imeweza kutoa mashirikiano katika
nyanja nyengine za kijamii, kiuchumi na kimaendeleo.
Nae aliyekuwa Mwakilishi Mkaazi huyo wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dk.
Tonia Kandiero alimueleza Dk. Shein kuwa Benki yake itaendelea kuiunga mkono
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutambua na kuthamini juhudi inazozichukua
katika kuleta maendeleo endelevu hapa nchini.
Dk. Kandiero alipongeza na kusifu mashirkiano mazuri yaliopo kati ya Benki hiyo na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Rais Dk. Shein na kueleza
kuwa hatua hiyo imesaidia sana katika kuleta maendeleo zaidi hapa Zanzibar.
Kiongozi huyo alimuhakikishia Dk. Shein kuwa miradi yote inayosimamiwa na Benki
hiyo itakamishwa ikiwemo miradi ya ujenzi wa barabara zikiwemo barabara ya
Mahonda -Mkokotoni yenye urefu wa km 31, Fuoni -Kombeni km 8.6, Pale- Kiongele
km 4.6 na Matemwe -Muyuni yenye urefu wa km 7.6.
Pamoja na hayo, Dk. Kandiero ambaye amefanya kazi zake hapa Tanzania kwa
takriban miaka sita, alimueleza Dk. Shein kuwa (AfDB) itaimarisha zaidi uhusiano na
ushirikiano wake na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kutoa pongezi za pekee
kwa Dk. Shein na serikali anayoiongoza kwa kusimamia vyema miradi ya maendeleo.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk