Você está na página 1de 3

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI


WAKALA WA VYUO VYA MAFUNZO YA MIFUGO - LITA

TANGAZO LA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA ASTASHAHADA NA STASHAHADA KATIKA WAKALA WA VYUO VYA MAFUNZO YA
MIFUGO (LIVESTOCK TRAINING AGENCY - LITA) KWA MWAKA WA MASOMO 2017/18

1. Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) inatangaza nafasi za mafunzo katika ngazi ya Astashahada na Stashahada kupitia Wakala wa
vyuo vya Mafunzo ya Mifugo.

2. Katika mwaka wa fedha wa 2017/2018 Serikali kupitia Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) itatoa mafunzo kwenye Kampasi zake
nane; Tengeru, Mpwapwa, Morogoro, Buhuri, Madaba, Temeke, Mabuki na Kikulula. Kampasi ya Temeke haina huduma ya malazi hivyo,
watakaojiunga itabidi wajitegemee. Pia katika Kampasi zetu wanachuo wa ufadhili binafsi watakaopenda kukaa nje ya Kampasi wanaruhusiwa.

3. Wakala inakaribisha maombi kutoka kwa vijana waliomaliza kidato cha nne wanaotaka kujiunga na mafunzo ngazi ya Astashahada (Cheti). Pia
vijana waliomaliza Kidato cha sita na wale wenye Astashahada (Cheti) katika fani zinazohusiana na kozi wanazoomba wanakaribishwa kwa ajili
ya kujiunga na mafunzo kwa ngazi ya Stashahada (Diploma).

4. Kozi zinazotolewa ni kama ifuatavyo :

Astashahada ya Afya na Uzalishaji Mifugo (Certificate in Animal Health and Production - CAHP)

Stashahada ya Afya na Uzalishaji wa Mifugo (Diploma in Animal Health and Production


DAHP)
Astashahada ya Ufundi Sanifu wa Maabara ya Veterinari (Certificate in Veterinary Laboratory
Technology - CVLT)
Stashahada ya Ufundi Sanifu wa Maabara ya Veterinari (Diploma in Veterinary Laboratory Technology
DVLT)
Stashahada ya Uendelezaji wa Nyanda za Malisho na Udhibiti wa Ndorobo (Diploma in
Range Management and Tsetse Control-DRMTC)
5. Kampasi zinazotoa mafunzo hayo ni kama zinavyoonekana katika jedwali hapa chini.

NA KAMPASI ANUANI SIMU KOZI ZITOLEWAZO


1. TENGERU S.L.P 3101 Arusha 0625874298 or 0727267335 DAHP & CAHP (Bweni na kutwa)
2. MPWAPWA S.L.P 51 Mpwapwa 0629635700 or 0627627519 DAHP & CAHP(Bweni na kutwa)
3. MOROGORO S.L.P 603 Morogoro 0752719458 or 0627885747 DAHP & CAHP (Bweni na kutwa)
4. BUHURI S.L.P 1483 Tanga 0757954229 or 0785271732 DAHP CAHP (Bweni na kutwa)
5. MADABA S.L.P 568 Songea 0784641501 or 0629102761 DAHP & CAHP(Bweni na kutwa)
6. TEMEKE S.L.P 39866 DSM 0754768877 or 0627627670 CVLT & DVLT (Kutwa)
7. MABUKI S.L.P 115 Misungwi 0712581367 or 0623984122 CAHP (Bweni na kutwa)
8. KIKULULA S.L.P 472 Karagwe 0763665322 or 0627627524 CAHP (Bweni na Kutwa)
9. LITA HQ S.L.P 9152 DSM 0627629505

6. Sifa za mwombaji
i. Stashahada ya Afya na Uzalishaji wa Mifugo (Diploma in Animal Health and Production
DAHP)
Awe amemaliza elimu ya Kidato cha Sita na kufaulu masomo mawili ya Sayansi kati ya Baiolojia, Kemia, Fizikia, Hisabati, Jiografia na
Kilimo. Kiwango cha chini cha ufaulu kitakachomwezesha muombaji kukubaliwa ni cha Principal pass moja na subsidiary moja
kwenye masomo ya sayansi. AU
Awe amemaliza mafunzo ya Astashahada (Certificate) katika fani ya Animal Health and Production (AHPC), CAHP NTA level 5, Agrovet au
Certificate in Agriculture and Livestock Production (CALP) waliosoma kwa mfumo wa muhula (term system)

ii. Stashahada ya Uendelezaji wa Nyanda za Malisho na Udhibiti wa Ndorobo (Diploma in


Range Management and Tsetse Control-DRMTC)
Awe amemaliza mafunzo ya Astashahada (Certificate) katika fani ya Animal Health and Production (AHPC- Term system) & CAHP NTA
level 5, Certificate in Agriculture and Livestock Production (CALP)

iii. Stashahada ya Ufundi Sanifu wa Maabara ya Veterinari (Diploma in Veterinary Laboratory Technology DVLT)

Awe amemaliza mafunzo ya Astashahada (Certificate) katika fani ya Veterinary Laboratory technology (CVLT) NTA level 5

iv. Astashahada ya Afya na Uzalishaji Mifugo (Certificate in Animal Health and Production - CAHP) na Astashahada ya Ufundi Sanifu wa
Maabara ya Veterinari (Certificate in Veterinary Laboratory Technology - CVLT)
Awe amemaliza Kidato cha Nne na kufaulu masomo mawili ya sayansi kati ya Baiolojia, Kemia, Fizikia, Hisabati, Jografia na Kilimo.
Kiwango cha chini cha ufaulu kitakachomwezesha muombaji kukubaliwa ni cha alama ya D kwenye masomo manne,(mawili ya sayansi
na mawili kwenye masomo mengine isipokuwa Dini na Upishi.
AU
Awe amesoma na kufaulu kidato cha nne na kujiendeleza katika vyuo vya ufundi VETA na kupata VTA Level 3 au Trade Test I.

7. Utaratibu wa kujaza fomu ya maombi


Mwombaji anaweza kuchukua fomu kutoka kwenye Kampasi (Chuo) au kwa kufungua Tovuti ya Wakala Website: http//www.lita.go.tz na
kujaza fomu na hatimaye kuzirudisha kwenye Kampasi (chuo) au kwa njia ya barua pepe zifuatazo: litahq@yahoo.com
Pamoja na fomu ya maombi ambatanisha payslip ya ada ya maombi uliyolipia kwenye akaunti ya Wakala kama ilivyoelekezwa kwenye fomu
ya maombi.
Zingatia: Maombi yoyote yasiyozingatia maelekezo tajwa katika tangazo hili hayatashughulikiwa
Fomu ya maombi (Application form) HAIUZWI!

8. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 15/08/2107.

10. Taarifa kwa watakaochaguliwa.

Majina ya watakaochaguliwa yatatolewa kwenye:

Website: www.lita.go.tz na magazeti ya Habari leo na Mwananchi.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na :

Mtendaji Mkuu,
Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo - LITA,
Veterinari Complex,
131 Barabara ya Nelson Mandela,
S. L. P 9152,
15487 Dar es Salaam

Simu Na. +255 22 28633479

Você também pode gostar