Escolar Documentos
Profissional Documentos
Cultura Documentos
Aprili 5, 2018
Dar es Salaam.
Nasema hivyo kwa sababu TEF inatoa matamko ambayo yanabeba sura
kuwa ni matamko ya waandishi wa habari wakati kiuhalisia siamini kuwa
huo ndio msimamo wa waandishi wa habari wa nchi hii.
1
Na mimi pia naomba nifanye hivyohivyo kwenye nyie Maaskofu wangu
yaani Jukwaa la Wahariri na kwa kweli nikulenge wewe Kaimu Mwenyekiti
wa TEF Deodatus Balile ambaye umelisoma tamko la TEF.
Ndugu Balile tamko lenu linatuletea maswali mengi kwenye jamii na hasa
Serikali ambayo ni sehemu muhimu ya kazi zetu za kila siku. Mimi nikiwa
mmoja wa waandishi wa habari ambao hawajashirikishwa na wala
hawajawahi kushirikishwa kwenye masuala ya TEF limenikwaza kwa
sababu wadau ambao nafanya nao kazi kwa karibu ni Serikali ambayo
kimsingi tamko lenu linaituhumu kwa mambo mazito yenye vinasaba vya
siasa za upinzani.
Sasa twende hoja kwa hoja, mosi, mnasema kuna sintofahamu katika hali ya
uchumi, mnazungumza hilo kwa kuzingatia nini? Maana takwimu
zinaonesha hali ya uchumi wa nchi yetu ni nzuri? Takwimu za hivi karibuni
zinaonesha kuwa uchumi wetu umepanda na sasa unakua kwa asilimi 7.1
kutoka 6.8, mfumuko wa bei umeshuka hadi asilimia 4.5, nchi yetu ni kati ya
nchi 5 zenye kasi kubwa ya kukua kwa uchumi barani Afrika.
Takwimu za Benki Kuu (BOT) zinaonesha nchi ina akiba ya fedha za kigeni
zaidi ya Bilioni 5 za kutosha kuagiza bidhaa na huduma kwa miezi 6 na Rais
kasema fedha za kutekelezea miradi mikubwa ya reli, kununua ndege,
barabara, maji, ujenzi wa viwanja vya ndege, elimu bure, kujenga flyover,
kujenga bandari, kununua dawa za hospitali na mengine, zipo. Rais kasema
Serikali ina fedha za kulipa mishahara wafanyakazi na haikopi katika
mabenki ya biashara kama ilivyokuwa zamani. Sasa nyie mnazungumza
sintofahamu ya kutoka wapi?
2
Balile na wenzako mnasema kuna sintofahamu ndani ya jamii kwa sababu
uhuru wa kutoa maoni unaminywa ukiwemo uhuru wa vyombo vya habari,
labda niulize wewe Balile gazeti lako la Jamhuri na mambo mazito
linayoyaandika kila toleo ni mahali gani umeminywa uhuru wako? Au
nimuulize Meena makala anazoandika kila siku kwenye magazeti
mbalimbali likiwemo Mwananchi, na jinsi zinavyoikosoa Serikali ni lini
uhuru wake umeminywa? Au Mwandishi wa habari mkongwe Jenerali
Ulimwengu na vijana wake akina Ezekiel Kamwaga jinsi wanavyotumia
gazeti lao la Raia Mwema kuandika mambo mazito ya kuikosoa Serikali ni
wapi uhuru wao unaminywa? Chukua magazeti ya leo Mwananchi, Tanzania
Daima, Nipashe, Mtanzania kwa kutaja machache soma na angalia kuna
habari ngapi zinaikosoa Serikali, umesikia yameminywa? Ipo mifano mingi.
Nilitarajia wewe Balile kwa elimu yako ya sheria ungekuwa mwalimu pale
ambapo waandishi wa habari wanadhani wana haki ya kuandika chochote tu
bila kutambua kuwa wana wajibu wa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni
mbalimbali zilizopo hapa nchini na pia kuzingatia weledi katika taaluma hii
ya uandishi wa habari.
Ningeelewa zaidi kama TEF katika tamko lenu mngesema pia kuhusu
makosa ya dhahiri ambayo vyombo vya habari vinayafanya na mara kwa
mara tunasoma Mkurugenzi wa Maelezo Dk. Hassan Abbas anavionya na
vinaomba radhi.
3
Tanzania tuwe hivyo? Mnakiona anachokifanya Ansibert Ngurumo akiwa
huko Finland au mmefumba macho hamsomi maandiko yake kwenye
mitandao ya kijamii?
4
zenu kutoa somo kwa wanahabari namna ya kufanya kazi kwa weledi katika
mikutano ya siasa iliyozuiliwa, sasa na nyinyi mmekuwa wanaharakati
mnadai vyama vya siasa vinaminywa, mnataka vikafanye mikutano
isiyoruhusiwa ili mtutume tukaandike habari halafu yatukute yaliyomkuta
Daudi Mwangosi?
Ndugu zangu njooni na solution sio kuja kulalamika. Halafu hebu kuweni
wakweli hata kabla ya nyakati hizi ni wakati gani waandishi wa habari
walikuwa na malipo mazuri na hali nzuri kazini? Tena nyie wenyewe
wahariri ndio mmekuwa wa kwanza kuwashawishi wamiliki wa vyombo vya
habari wawalipe waandishi shilingi 1,750/= kwa habari inayotumwa
gazetini, yaani mwandishi wa habari anaitafuta habari tena kwa kusafiri kwa
gharama kubwa na mwisho wa siku malipo yake ni shilingi 1,750/=, nyinyi
wenyewe wahariri ndio ambao mnapokea habari kutoka kwa waandishi wa
habari ambao hawana mishahara, hawana ajira, hawana mikataba ya kazi na
hata hawana mafao yoyote. Na haya mambo hayajaanza leo.
5
Waandishi wa habari wanafariki dunia, tunaishia kuchangisha fedha ili
kununua hadi chakula cha watu waliopo msibani. Lakini nyie TEF hata siku
moja hatujawaona mkiwabana hao wamiliki wabebe majukumu ya
kuhudumia wafanyakazi wao wanapoumwa ama kifo.
Najua baada ya kuandika maoni yangu haya mtakuja kusema sijui katiba ya
TEF na nimeandika takataka lakini nataka niwaambie turudi kwenye misingi
yetu, acheni kutupeleka kwenye mwelekeo unaoharibu taswira ya tasnia hii
ya habari. Msituingize kwenye siasa, hii ni taaluma inayoheshimika duniani
kote. Inawezekana nyie mna maslahi yenu lakini ndani ya tasnia hii tumo
ambao tunategemea kalamu na weledi wetu, msituyumbishe na
msitugombanishe na Serikali.
6
sasa duniani kote inasifika kwa kuwa na kiongozi Mhe. Rais John Pombe
Magufuli ambaye ni mfano bora wa kuigwa barani Afrika kwa juhudi zake
za kutetea wanyonge, kupigania rasilimali za nchi, kupiga vita rushwa,
kubana matumizi yasiyo ya lazima, kujenga viwanda na kujenga uchumi
imara wa kutupeleka katika kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.